top of page

Mwili Wangu
Ni
Mwili Wangu

Bure Muziki Kuzuia Watoto Kuzuia Programu

Ishara za dhulma dhidi ya watoto

Zifutazo ni ishara za dhulma au upuuzaji ambazo huenda ukaziona na watoto. Iwapo utaziona ishara hizi ama mtoto akujulishe jambo Fulani:
 

1. Kuwa mtulivu na usimlazimishe akuambie zaidi.

2. Mfariji mtoto huyo na umshukuru kwa ajili ya kukujulisha, kisha uyajulishe Mashirika husika ya Huduma za Kuwalinda Watoto.

3. Kumbuka kuwa mtoto huenda akakupa tu asilimia ndogo ya habari kila wakati hadi watakaporidhika kuwa wewe ni mtulivu na unampa usaidizi.
 

Zifuatazo ni ishara za dhulma. Huenda mtoto anatatizika na baadhi ya dhulma hizi hivyo basi huu ni mwongozo tu. Endapo utatambua mabadiliko makuu katika tabia za mtoto hakikisha kuwa umeyazingatia na uone iwapo yafuatayo yanalingana.


Ishara za dhulma za kimwili.  

Anavyoonekana mtoto.

*michibuko isiyo ya kawaida, lengelenge, kuvunjika

*alama za meno katika sehemu alizoumwa
*majeraha ambayo husingiziwa kutokana na ajali
*endapo maelezo hayatalingana na jeraha
*kuvalia mavazi marefu ili kuficha majeraha tabia ya watoto
*asiyeeleweka
*wenye woga usio wa kawaida, na huwaepuka watu wengine
*aliye na hamu kuu ya kuwapendeza wengine
*aonekanaye kuwaogopa wazazi

*aonekanaye kutojali anapotenganishwa na wazazi.
 

Ishara za kupuuzwa

Aonekanavyo mtoto

*mchafu, nywele chafu,
*anukaye vibaya
*aliye na mavazi yasiyoambatana na hali ya anga
*anayehitaji matibabu

 

Tabia ya mtoto

*aliye na uchovu kwa wakati mwingi
*aliye na tabia ya kuba au kuomba chakula
*akosaye kuenda shuleni siku nyingi au achelewaye wakati mwingi
*mtoto asiyetii amri
*asiyejiamini o

Ishara za dhulma za Hisia

Aonekanavyo mtoto
Huenda ishara hizi zikakosa kuwa bainifu kama zilivyo katika hali zingine, tabia huenda zikawa ishara bora zaidi.

*kujitenga na marafiki
*akosaye kuenda shuleni siku nyingi au achelewaye wakati mwingi
*asiyejiamini
*asiyetii amri
*mabadiliko katika masomo yake

Ishara za dhulma za kingono
 

Aonekanavyo mtoto

*mavazi ya ndani yaliyoraruka na yenye matone ya damu.
*anayehisi uchungu katika sehemu zake za siri
*aliye na magonjwa ya zinaa

Tabia za mtoto

Kwimbonakalo yomntwana

*tabia za kingono au maarifa ambayo yasiyolingana na umri wake
*kuwashika watoto wengine kwa njia isiyofaa
*mabadiliko ya ghafla ya tabia
*kuzuia vikali kushikwa kwa njia yoyote ile

Endapo utashuku dhulma dhidi ya mtoto, yajulishe Mashirika husika ya Huduma za Kuwalinda Watoto ili kupata ushauri unaofaa. Watayasikiliza matakwa yako na kuchukua hatua kwa niaba yako iwapo mtoto yu hatarini.

Tuwalinde watoto!!
 

Mwili Wangu Ni Mwili Wangu.
 

Nakala hii imeandikwa na kuhuishwa na 

Chrissy Sykes © 2017

Tafsiri : JB Mugi
 

bottom of page